Watu 15 wamepigwa risasi na kufariki dunia papo hapo, baada ya mtu mwenye silaha kuyashambulia mabasi miwili madogo ya abiria nchini Afghanistan.
Mtu huyo anayedhaniwa ni kutoka kundi la Taliban, alifanya shambulio hilo wakati watu hao walipokuwa wakisafiri kwa barabara katika jimbo la Ghor nchini Afghanistan.
Kwa mujibu wa taarifa toka kwa maafisa wa polisi wa jimbo hilo, mtu huyo mwenye silaha aliyasimamisha mabasi hayo, akawaamuru abiria wote kushuka chini, kisha akaanza kuwamiminia risasi na kuwaua wote.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni