Mke wa bingwa wa zamani wa mbio za
magari za Langalanga Michael Schumacher, Corina ametangaza kuiuza
ndege ya mumewe Schumacher ambayo alikuwa akiitumia kuisafiria katika
maeneo mbalimbali dunia, kwa kiasi cha paundi milioni 12.
Kuuzwa kwa ndege hiyo siku 207
kupita tangu maisha ya Schumacher kubadilika kwa ajali ya kuteleza
kwenye barafu huko Ufaransa katika Mlima Alps inaonekana kama ni
ushahidi kuwa Michael hataweza tena kukabiliana na mikiki mikiki ya
safari.
Schumacher, yupo katika hali ya
kushindwa kutembea katika kliniki ya Lausanne huko Switzerland akiwa
anafanyiwa mazoezi ya viungo na mishipa iliyopata hitilafu baada ya
kuangukia kichwa wakati akiteleza kwenye barafu Desemba 29 mwaka
jana.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni