Zaidi ya abiria 17 waliokuwa wakisafiri na basi la kampuni ya Morobest kutoka wilayani Mpwapwa mkoni Dodoma kuelekea jijini Dar es Salaam wamefariki dunia huku wengine zaidi ya 50 wakijeruhiwa baada ya basi hilo kugongana na lori la mizigo katika eneo la Pandambili, Dodoma.
Chanzo cha habari kinasema kuwa, chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa lori aliyekuwa akitaka kulipita lori lingine, ndipo lilipo gongana uso kwa uso na basi hilo. Madereva wote wawili ni kati ya waliopoteza maisha katika ajali hiyo.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni