Benki ya Dunia imetangaza kutenga
dola milioni 200 kwa ajili ya msaada wa dharura kwa nchi za Afrika ya
Magharibi ili kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.
Fedha hizo zitatolewa kwa serikali
za Liberia, Sierra Leone na Guinea pamoja na kwa Shirika la Afya
Duniani (WHO).
Idadi ya watu waliokufa kutokana na
mlipuko wa ugonjwa huo hatari imefikia watu 887, kwa mujibu wa WHO.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni