Wanamuziki wanandoa Beyoncé na Jay
Z, wanapanga kuendelea na tamasha la mwisho la pamoja Jijini Paris
nchini Ufaransa ambalo litarekodiwa na HBO maalum mwezi ujao, licha
ya uvumi wa kuvurugika kwa mahusiano yao.
Mahusiano ya wanandoa hao nyota
yanasemekana yapo katika mgogoro mkubwa kiasi cha wanasheria wa
promota wa tamasha lao la Live Nation kuitwa katika mkutano wa
kutafuta ufumbuzi wiki iliyopita.
Hata hivyo tamasha hilo
litakalofanyika katika Jiji la mapenzi wa Paris litaendelea kama
kawaida kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na HBO na tarehe itakuwa
Septemba 20, mwaka huu.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni