Mfaransa Herve Renard ameteuliwa na shirikisho la soka la Ivory Coast kukionoa kikosi cha timu ya taifa ya nchi hiyo.
Renard anachukua nafasi ya Sabri Lamouchi ambaye alijiuzulu kuendelea kuifundisha timu ya taifa ya Ivory Coast baada ya kumalizika kwa fainali za kombe la Dunia zilizofanyika nchini Brazil mwaka huu.
Renard mwenye miaka 45 alikuwa ikiifundisha timu ya taifa ya Zambia, na mwaka 2012 aliipeleka timu hiyo katika fainali za Mataifa ya Afrika.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni