Nchi ya Ivory Coast imetangaza
kupiga marufuku ndege zote zinazotoka kwenye nchi zinazokabiliwa na
mlipuko wa ugonjwa hatari wa Ebola ikiwa ni hatua za kukabiliana na
jitihada za kudhibiti ugonjwa huo kuingia nchini humo.
Serikali imesema imekataza ndege za
abiria kutoka nchi hizo kuja Ivory Coast hadi hapo itakapotolewa
agizo lingine, na pia imezuia shirika la ndege la taifa la Cote
d'Ivoire kwenda katika nchi hizo.
Taarifa hiyo haikutaja nchi hizo
lakini takwimu zinaonyesha watu 1000 wamekufa kwa kuugua ugonjwa wa
Ebola katika nchi za Liberia, Sierre Leone, Guinea pamoja na Nigeria.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni