Kesi ya mauaji inayomkabili
mwanariadha wa Afrika Kusini Oscar Pistorius inatarajiwa kukamilisha
malumbano ya kisheria baada ya kumalizika kwa utoaji wa ushahidi
katika kesi hiyo inayofuatiliwa mno na vyombo vya habari vya ndani na
nje.
Mwendesha mashtaka Gerrie Nel
atakuwa wa kwanza kumalizia kutoa maelezo yake, ambapo upande wa
utetezi nao utafuatia kufanya hivyo hapo kesho.
Mwanariadha huyo mlemavu amekanusha
kumuua kwa makusudi rafiki yake wa kike mwanamitindo Reeva Steenkamp
Februari 14 mwaka jana na kudai kuwa alidhani kuwa ni mtu aliyevamia
nyumbani kwake.
Reeva akiwa na mpenzi wake Pistorius wakati wa uhai wake


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni