Nchi ya Liberia itapokea dawa ambayo
haijafanyiwa majaribio ya Zmapp, ili kuwatibu watu wanaougua ugonjwa
hatari wa Ebola.
Rais wa Liberia Ellen Johnson
Sirleaf, amesema hatua hiyo inatokana na ombi la nchi yake kwa
Marekani ili kupatiwa dawa hizo.
Hatua hiyo imekuja wakati wataalamu
wa tiba wakikutana Jijini Geneva katika kujadili namna ya kutumia
tiba hiyo mpya ya dawa za Zmapp.
Shirika la Afya Duniani (WHO) ambalo
ndio mwenyeji wa mkutano huo limesema jumla ya watu 1,013 wamekufa
kwa ugonjwa wa Ebola Afrika Magharibi.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni