Timu ya Manchester United
imethibitisha kunasa saini ya mchezaji wa Sporting Lisbon beki Marcos
Rojo kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 16.
Rojo, ambaye alitua jumanne jioni
Jijini Manchester na kusema kujiunga na Manchester United kwake ni
sawa na kukamilisha ndoto yake ametia saini jana mkataba wa miaka
mitano baada ya kufaulu vipimo na kukubaliana na maslahi yake.
Kocha Louis van Gaal amehakikisha
kuwa anamnasa beki huyo anayetumia mguu wa kushoto, kufuatia kupata
kipigo jumamosi kutoka kwa Swansea, katika mchezo wa Ligi Kuu ya
Uingereza.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni