Idadi ya watu waliofariki dunia kutokana na maporomoko ya ardhi yaliyosababishwa na mvua kubwa nchini Japan imefikia 39 huku msako wa kuwatafuta watu wengine waliopoteza maisha ukiendelea kwa kasi.
Idadi hiyo ya waliopoteza maisha imeongezeka kufuatia msako wa kuondoa vifusi katika maeneo hayo yaliyokumbwa na maporomoko katika safu za milima ya Hiroshima.
Shirika la utabiri wa hali ya hewa la Japan limesema maporomoko hayo kwenye milima ya Hiroshima yalisababishwa na mvua kubwa iliyonyesha kwa saa 24 na ambayo ilikuwa ni sawa na mvua iliyonyesha kwa muda wa mwezi mmoja mfululizo.
Picha toka eneo la tukio zinaonyesha nyumba zikiwa zimefukiwa na matope pamoja na mawe yaliyotokana na maporomoko hayo, wakati vikosi vya uokoaji vikiwa vinaelekea katika nyumba zilizobomolewa na kufunikwa na matope.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni