Mwanaume mmoja nchini Marekani
ametekelezewa adhabu yake ya kifo katika jimbo la Missouri baada ya
kutiwa hatiani kwa kosa la kubaka na kumuua mwanafunzi wa chuo mnamo
mwaka 1995.
Adhabu hiyo imetekelezwa kwa Michael
Worthington, 43, ni ya kwanza kutekelezwa Marekani tangu mwezi
uliopita, ambapo dawa ya sindano ya kifo kwa mfungwa huko Arizona
ilipochukua muda wa saa mbili kabla ya kufa.
Worthington alikiri kumshambulia,
kumbaka na kumuua mwanafunzi Melinda Griffin, 24, akiwa nyumbani
kwao. Ilimchukua muda wa dakika 10 kabla ya Worthington kufa baada ya
kuchomwa sindano hiyo ya kifo.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni