Meriam alihukumiwa kunyongwa mapema mwaka huu na mahakama nchini Sudan baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kubadili dini, alisalimika baada ya mataifa mbalimbali ulimwenguni ikiwemo Marekani kupinga hukumu hiyo.
Meriam na mumewe ni wazaliwa wa Sudan lakini wenye uraia wa Marekani.
Akiwa gerezani alijifungua mtoto wake mdogo, na hata alipotoka gerezani bado alikumbana na vikwazo mbalimbali kabla ya kupata hifadhi katika ubalozi wa Marekani nchini Sudan.
Baadaye alifanikiwa kuondoka nchini humo na kuelekea Rome, Italia ambako huko alikutana na kiongozi wa Kanisa Katoliki Dunia, Papa Francis, na hadi kuwasili Marekani jana alhamisi alikuwa akitokea Italia yeye na familia yake.
Walipowasili nchini Marekani, walipokelewa kwa furaha na ndugu na jamaa zao, hali iliyomfanya mumewe Meriam, Daniel Wani atokwe na machozi mfululizo.




Hakuna maoni :
Chapisha Maoni