Chama cha Kisoshalisti cha Brazil
(PSB) kimemtangaza rasmi mwanaharakati wa kimataifa wa mazingira Bi.
Marina Silva kuwa mgombea wake mpya wa urais.
Bi. Silva anachukua nafasi ya
marehemu Eduardo Campos ambaye alikufa katika ajali ya ndege wiki
iliyopita.
Mwanamazingira huyo alikuwa ni
mgombea mwenza wa marehemu Campos, na alikuwa ni waziri wa manzingira
katika serikali ya Brazil.
Bi. Silva anaonekana kuwa ataleta
ushindani mkubwa kwa rais Dilma Rousseff, ambaye anawania kuchaguliwa
tena katika uchaguzi utakaofanyika Oktoba 5, mwaka huu.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni