Timu ya Manchester United na
Liverpool zinakutana leo Jijini Florida nchini Marekani katika mchezo
wa kirafiki, ambao kutokana na upinzani wao mchezo huo unaonekana
kama si wa kirafiki bali ni wa kuchukuliwa kwa umakini mno ili
kulinda heshima.
Katika msimu uliopita Liverpool
iliifunga Manchester United mabao 3-0, na kumaliza msimu wa ligi hiyo
ikiwa na pointi 20 zaidi ya wapinzani wao hao wanaonolewa hivi sasa
na kocha Louis van Gaal.
Kocha Van Gaal amesema atatangaza
wachezaji ambao hawahitaji katika kikosi cha Manchester United baada
ya kumalizika kwa mchezo huo, ambao unakamilisha ratiba za michezo ya
kirafiki kwa klabu hiyo kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu ya Uingereza.
Wachezaji wa Manchester United wakijifua


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni