Kivuko kilichokuwa na abiria 200
kimezama kusini magharibi mwa Bangladesh katika Jiji la Dhaka.
Watumishi wa Uokoaji wa Dharura
pamoja na wanajeshi wamefika katika tukio la ajali hiyo wilaya ya
Mushiganj, ambapo ndipo ajali ilipotokea kwenye mto Padma kilomita 30
kutoka Jiji la Dhaka.
Taarifa zinasema watu 50 wameokolewa
kutoka katika kivuko hicho cha Pinak 6.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni