Ndege iliyokuwa imejaa abiria
wakielekea Manchester imelazimika kutua kwa dharura katika uwanja wa
ndege wa jeshi unaolindwa kwa silaha huko Azores baada ya injini yake
moja kuzimwa.
Wakati hitilafu hiyo ikitokea ndege
hiyo ya Thomson Airways Boeing 787 Dreamliner
ilikuwa na abiria 288 wanaotokea
Jamhuri ya Dominica ambapo waliambiwa na rubani injini moja itazimwa
kutokana na hitilafu.
Baada ya kutolewa taarifa hiyo
abiria waliambiwa ndege itatua kwa dharua katika uwanja ulipo karibu
na baada ya kusafiri ikiwa kima cha chini kwa saa nne, walielezwa
wajiandae kutua katika mazingira magumu kwenye uwanja huo wa jeshi.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni