Mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini
Oscar Pistorius ameshutumiwa kwa kuwa shahidi muongo ambaye ameiambia
mahakama rundo la maelezo ya uongo, kauli ambayo imetolewa wakati wa
kukamilisha malumbano ya kisheria ya kesi ya mauaji inayomkabili.
Wakati Pistorius akikanusha kumua
kwa makusudi mpenzi wake Reeva Steenkamp kwa madai ya kufikiri kuwa
ni mtu aliyevamia nyumbani kwake, hata hivyo mwendesha mashtaka
amesema alimuua kwa makusudi baada ya kugombana.
Mwendesha mashtaka huyo Gerrie Nel,
ametoa maelezo hayo wakati akikamilisha kutoa maelezo yake katika
kesi hiyo hii leo, kabla nao upande wa utetezi kutoa maelezo yake
hapo kesho.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni