.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 7 Agosti 2014

PADRI MMOJA RAIA WA UFARANSA AUGUA EBOLA NA KUREJESHWA HISPANIA

Padri raia wa Hispania amekuwa ni mtu wa kwanza aliyeugua Ebola kurejeshwa nyumbani barani Ulaya kwa ajili ya matibabu hii leo.


Padri Miguel Pajares, amekimbizwa hospitali Jijini Madrid, baada ya kubebwa kwa ndege ya jeshi akitokea nchini Liberia leo asubuhi.

Mmishenari huyo alibidi atengwe na watu tangu jumamosi, baada ya kubainika anavirusi vya ugonjwa hatari wa Ebola.

Padri Pajares, ambaye alikuwa akitibu wagonjwa wa Ebola katika hospitali inayo milikiwa na Kanisa Katoliki, amerejeshwa na sista aliyeambatana nae ambae naye yupo chini ya uangalizi wa madaktari ingawa hajaambukizwa virusi vya ugonjwa huo.
                     Picha ya ndani ya ndege ya jeshi iliyombeba Padri Pajares
Mgonjwa wa Ebola akiwa amelala chini nje ya kituo cha kupimia huko Guinea
       Vilio vikiwa vimetawala kwa ndugu na jamaa wenye wagonjwa wa Ebola

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni