Watu wanne wamekufa kwa njaa huko
Baragoi, kaunti ya Samburu kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na
Chama cha Msalaba Mwekundu nchini Kenya.
Mratibu wa chama hicho Gitonga
Mugambi katika ukanda huo ameviambia vyombo vya habari mzee mmoja
amekufa wiki iliyopita.
Hata hivyo wakazi wa eneo hilo
wamedai watu saba wamekufa kwa njaa, miongoni mwao wapo wanawake
wanne, mtoto mmoja na wanaume wawili katika eneo la Logetei huko
Baragoi.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni