.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 7 Agosti 2014

RAIS WA LIBERIA ATANGAZA HALI YA TAHADHARI KATIKA TAIFA HILO KUTOKANA NA EBOLA

Rais wa Liberia Ellen Johnson Sirleaf ametangaza hali ya dharura wakati taifa hilo likikabiliwa na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.

Akiongea kwenye televisheni ya taifa amesema baadhi ya uhuru wa raia kujifanyia mambo watakavyo utasitishwa.

Ugonjwa wa Ebola umezikumba nchi za Guinea, Sierra Leone na Nigeria, huku ukiuwa watu zaidi ya 930.

Wataalam wa Shirika la Afya Duniani (WHO) wanakutana Jijini Geneva nchini Switzerland, kujadili namna ya kukabiliana na mlipuko huo mkubwa kuwahi kutokea.


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni