China imetuma wanajeshi 2,500 katika
mkoa wa kusini magharibi katika mkoa wa Yunnan, baada ya tetemeko
lardhi kuua mamia ya watu.
Watu wapatao 381 wamekufa na wengine
zaidi ya 1,800 wamejeruhiwa baada ya tetemeko hilo lenye ukubwa wa
6.1 kutokea hapo jana.
Kikosi cha jeshi la China wakiwa na
vipimo vya kubaini mtu aliyehai wanaelekea katika mkoa huo kusaidia
jitihada za uokoaji watu kwenye mkoa huo.



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni