Marekani imetangaza mpango wa kutuma
wataalam wa afya 50 Afrika Magharibi kusaidia kukabiliana na
mlipuko hatari wa ugonjwa wa Ebola.
Afisa Mwandamizi wa Afya wa Marekani
amesema mlipuko huo wa Ebola unaonekana kushindwa kudhibitiwa na
kusisitiza lazima udhibitiwe.
Ugonjwa wa Ebola umeshauwa watu 728
katika nchi za Guinea, Liberia na Sierra Leone tangu kutokea kwa
mlipuko wake.
Wakati huo huo daktari wa Marekani
aliyeambukizwa Ebola anaendelea vizuri tangu arejeshwe Marekani
akitokea Liberia.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni