Nchi ya Israeli imetangaza kusitisha
mapigano kwa saa saba kwa ajili ya utoaji huduma za misaada ya
kibinadamu huko Gaza kuanzia leo asubuhi.
Afisa Mwandamizi wa Jeshi la Israeli
amesema usitishaji mapigano hayo hautahusisha mji wa Rafah, na
kuongeza kuwa wanajeshi wake watajibu mapigo iwapo watashambuliwa.
Mapema Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban
Ki-moon alielezea kitendo cha Israeli kushambulia shule ya Umoja wa
Mataifa huko Gaza kama si chauadilifu na ni kitendo cha uhalifu.
Shambulio katika shule hiyo
limeelezwa na Mamlaka za Palestina kuwa limesababisha vifo vya watu
10, hapo jana.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni