.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 21 Agosti 2014

WANAJESHI WASAMBAZWA LIBERIA KUSIMAMIA AMRI YA KUTOTOKA NJE

Vikosi vya Ulinzi vya nchini Liberia vimesambazwa katika Jiji la Monrovia kusimamia marufuku ya kutotoka mtu kwenye kitongoji kikubwa cha makazi duni katika jitihada za kudhibiti ugonjwa hatari wa Ebola.

Hatua hiyo imechochea maandamano ya kupinga marufuku hiyi kutoka kwa wakazi wa kitongoji hicho cha West Point ambapo watu wamekusanyika katika vizuizi vya barabarani kulalamikia agizo hilo.

Rais Ellen Johnson Sirleaf pia ameagiza kutotoka nje watu usiku ikiwa miongoni ya mikakati ya kukabiliana na Ebola, ambayo imeua watu 1,350 tangu kutokea mlipuko wake kwenye nchi nne za Afrika ya Magharibi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni