Kamanda wa polisi wa mkoa wa Arusha Lebaratus Sabas amewataja waliopoteza maisha kuwa ni pamoja na dereva wa basi dogo aliyejulikana kwa jina la Jumanne Mohamed na abiria aliyejulikana kwa jina la Anaret Sabas.

Mganga mkuu wa wilaya ya Arumeru walikolazwa majeruhi Dr, Azizi Msuya amesema majeruhi wanaendelea na matibabu na kwamba baadhi yao wamepelekwa katika hosipitali ya mkoa ya Mount Meru .

Mganga mkuu wa wilaya ya Arumeru walikolazwa majeruhi Dr, Azizi Msuya amesema majeruhi wanaendelea na matibabu na kwamba baadhi yao wamepelekwa katika hosipitali ya mkoa ya Mount Meru .
Kwa mujibu wa watu walioshuhudia ajali hiyo wamesema imetokea baada ya basi la Hood kutaka kulipita gari lingine .
Basi la Hood lilikuwa linatoka Arusha kwenda Mbeya na basi dogo aina ya Hiace lilikuwa linatoka Usa river kwenda jijini Arusha

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni