WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe amekutana na Mwanaharakati wa Kimataifa wa haki za wanawake na watoto, Graca Machel na kujadili masuala mbalimbali ya haki za wanawake na watoto katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo.
Katika
mazungumzo yao, Waziri Chikawe alimwambia mke huyo wa Rais wa zamani
wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, juhudi zake za kuingiza katika
Katiba Mpya kifungu cha kuzuia mtoto wa chini ya miaka 18 asioe wala
asiolewe.
Hata
hivyo, Mama Machel kwa upande wake alimshukuru Waziri Chikawe kwa
maoni yake na kusema kuwa ni muhimu kwa wadau wote wa haki za watoto
wakashinikiza wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba na watunga sheria
wote wahakikishe kipengele hicho kinaingia ndani ya Katiba. Mama
Machel yupo nchini kuhudhuria mkutano wa ufunguzi wa Kampeni ya
Kitaifa
ya
kutokomeza ndoa za utotoni.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni