Kinda wa Manchester United Adnan
Januzaj amepachika kimiani mabao matatu yaani hat-trick wakati kocha
Louis van Gaal akishuhudia kikosi cha timu hiyo cha wachezaji wa umri
wa chini ya miaka 21.
Katika mchezo huo beki Luke Shaw
aliyesajiliwa na Manchester United katika msimu huu naye alicheza,
wakati klabu hiyo iliibuka na ushindi wa mbao 4-0 dhidi ya
Sunderland.
Kocha Van Gaal akiangalia vitu vya Adnan Januzaj
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni