Cristiano Ronaldo amepachika mabao
matatu kimiani yaani hat-trick huku akisaidiwa na Gareth Bale
kuifanya Real Madrid kuichakaza Deportivo La Coruna kwa mbao 8-2
katika mchezo wa La Liga.
Mshambuliaji huyo raia wa Ureno
Ronaldo alipachika kimiani mabao mawili katika kipindi cha kwanza na
James Rodriguez kufunga moja na kufanya matokeo kuwa Real kuwa mbele
kwa mabao 3-0 hadi mapumziko.
Ronaldo alikamilisha hat-trick yake
katika kipindi cha pili, huku mchezaji wa Manchester United
aliyotolewa kwa mkopo Real Javier Hernandez akicheka na nyavu mara
mbili katika dakika za mwisho.
Gareth Bale akifunga goli lake la kwanza kati ya mawili aliyoyapachika wavuni
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni