Jaji katika kesi inayomkabili
mwanariadha mlemavu Oscar Pistorius leo anatarajiwa kukamilisha kutoa
hukumu yake iwapo mwanariadha huyo wa Afrika Kusini alimuua bila ya
kukusudia mpenzi wake.
Jaji Thokozile Masipa jana
alimsafisha mwanariadha huyo dhidi kosa la kuua kwa kukusudia, kwa
kusema wendesha mashtaka walishindwa kudhibitisha alimua kwa makusudi
mwanamitindo Reeva Steenkamp mwaja jana.
Pistorius alikiri kufyatua risasi
kwenye mlango wa choo chake lakini alisema alidhania kuwa kunamtu
kamvamia nyumbani kupitia chooni na wala hakuwa anajua kuwa ni mpenzi
wake Steenkamp.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni