.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 12 Septemba 2014

MUINGEREZA ALIYEUGUA EBOLA NA KUPONA AJIPANGA KUREJEA TENA SIERRA LEONE

Muingereza wa kwanza kupata maambukizi ya Ebola katika mlipuko wa sasa barani Afrika anatarajia kurejea katika nchi ambayo ndipo alipopata maambukizo ili kusaidiana na wenzake kupambana na ugonjwa huo.

Muingereza huyo William Pooley mwenye umri wa miaka 29 alitibiwa Jijini London baada ya kusafirishwa kwa ndege kutokea Sierra Leone baada ya kupata maambukizi ya ugonjwa huo hatari.

Baada ya kupatiwa tiba nyumbani Uingereza sasa Pooley amepona na kuruhusiwa kutoka hospitali na amesema anatarajia kurejea Sierra Leone katika wiki chache ili kusaidia tena kukabiliana na mlipuko wa Ebola.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni