Aliyekuwa kiogozi wa chama cha siasa
cha Democratic Change nchini Uganda Kanali Kizza Besigye amekutana na
kijana Jeff Ochieng kutoka Kenya ambaye anafanana mno na mwanasiasa
huyo maarufu.
Ochieng mwenye umri wa miaka 22
amekuwa akimtafuta baba yake mzazi kwa miaka tisa sasa tangu mama
yake afariki dunia na amekuwa akijiuliza iwapo Kanali Besigye ni baba
yake mzazi.
Kijana Ochieng mwenye miaka 22,
aliwasili Uganda kumuuliza Kanali Besigye iwapo wanauhusiano lakini
baada ya maelezo yao ya muda mrefu, imebainika kuwa hakuna uwezekano
wa Ochieng kuwa mtoto wa Kanali Besigye.
Kanali Kizza Besigye akiwa na familia yake
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni