.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 20 Septemba 2014

KINANA, NAPE WAITEKA KIBAHA


Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakiwasalimia wakazi wa Kibaha mjini wakati wakiwasili kwenye uwanja wa mkutano.


Kikundi cha ngoma cha Kisamamwe kikitumbuiza ngoma ya Afrika kabla ya kuanza kwa mkutano wa hadhara ambapo Katibu Mkuu wa CCM alihutubia wananchi wa Kibaha mjini.


Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Kibaha mjini ambapo aliwaambia wapinzani wamekosa hoja ya msingi kiasi cha kuamua kufanya maandamano ya kuleta vurugu nchini.


Sehemu ya Umati wa watu wakisikiliza mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.


Mbunge wa Kibaha mjini Silvestry Francis Koka akihutubia wakazi wake na kuwaambia kuwa pamoja na jitihada zote anazofanya maji bado ni donda sugu ila ufumbuzi upo njiani.


Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Kibaha mjini wakati wa mkutano wa hadhara ambapo aliwaambia viongozi wa halmashauri hawana budi kukaa na wafanya biashara ndogo ndogo kujadili kodi kabla ya kuwapangia kuona kama wana uwezo wa kulipa ama hapana hii itasaidia kupunguza lawama na mikingamo baina ya wafanya biashara na halmashauri.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni