Mchezaji wa zamani wa Chelsea, Frank Lampard alizima kabisa ndoto za kocha Mreno Jose Mourinho na kikosi chake cha Chelsea kuondoka na ushindi wa pointi tatu katika uwanja wa Etihad, pale alipofunga bao la kusawazisha na kufanya matokeo kuwa 1-1 hadi mpira unamalizika.
Mchezaji huyo mtokea benchi alifunga bao lake la kwanza msimu huu akiwa na Manchester City katika dakika ya 85 ya mchezo huo wa ligi kuu Uingereza uliochezwa jana.
Chelsea ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya 71 ya mchezo, bao hilo likifungwa na Andre Schurrle.
Mlinda mlango wa Chelsea akiruka bila mafanikio kuokoa mpira uliopigwa na Frank Lampard na kujaa moja kwa moja nyavuni.
SAWA NIMEFUNGA, SISHANGILIII!! Frank Lampard pamoja na kufunga bao hilo muhimu hakuashangilia kama ishara ya heshima kwa Chelsea, timu aliyopata kuichezea kwa mafanikio makubwa na kutwaa mataji mbalimbali.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni