.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 22 Septemba 2014

SIERRA LEONE YAMALIZA SIKU TATU ZA KUTOTOKA NJE KUKABILIANA NA EBOLA

Siku tatu za kutotoka nje ili kudhibiti mlipuko wa Ebola nchini Sierra Leone zimeelezwa kuwa zimekuwa na mafanikio na mamlaka za nchi hiyo.

Agizo hilo la kutotoka nje katika maeneo mengi ya nchi hiyo limemalizika jana usiku, na halitaongezwa muda kwa mujibu wa mamlaka za Sierra Leone.

Sierra Leone ni moja ya nchi ambazo zimeathiriwa mno na mlipuko wa Ebola, ikiwa na vifo 550 kati ya vifo 2,600 vilivyotokea hadi sasa.

Wakati huo huo nchi ya jirani ya Liberia imetangaza kuongezeka mara nne kwa wagonjwa waliolazwa kutokana na mlipuko wa Ebola.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni