.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 22 Septemba 2014

UTURUKI YAFUNGA MIPAKA YAKE NA SYRIA BAADA YA KUPATA WAKIMBIZI 70,000

Uturuki imeanza kufunga mipaka yake na Syria baada ya wakimbizi 70,000 wa Kikurdi kuingia nchi hiyo siku ya Ijumaa.

Hali hiyo imechangiwa na mapambano ya siku ya Jumapili baina ya vikosi vya usalama vya Uturuki na Wakurdi waliokuwa wanapingana nao.

Kufungwa kwa mipaka kutawazuia Wakurdi walio Uturuki kurejea Syria kupambana na wapiganaji wa kundi la Dola ya Kiislam (IS).

Wengi wa wakimbizi wanaotokea mji wa Kobane, wamekimbia mauaji yanayofanywa na wapiganaji wa kundi la IS ambao wamekuwa wakisonga mbele kuutwaa mji huo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni