Msako umeanza huko Lima, Ohio nchini
Marekani baada ya kijana mmoja nchini Marekani ambaye aliwapiga
risasi na kuwauwa wanafunzi watatu, kutoroka gerezani.
Kijana huyo TJ Lane, 19, anatumikia
adhabu ya vifungo vitatu vya maisha baada ya kukiri kosa la mauaji
katika shule ya Chardon Februari 2012.
Polisi wamesema mfungwa mwingine
aliyetiwa hatiani kwa kosa wizi, Clifford Opperud, pia naye ametoroka
katika tukio hilo.
Mamlaka za Marekani zimesema
haziamini kama wafungwa hao wanasilaha lakini wawili hao ni watu
hatari.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni