.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 19 Septemba 2014

PPF YAWANOA WAAJIRI KUHUSIANA NA HUDUMA ZAKE MPYA IKIWEMO PPF TAARIFA APP


Prof. Betria Mapunda ambae amemwakilisha Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar Es salaam akifungua semina iliyoandaliwa na Mfuko wa Pensheni wa PPF kwa Waajiri kwa lengo la Kutoa elimu juu ya huduma zitolewazo na mfuko huo wa Pensheni wa PPF katika ukumbi wa Seaescape, Uliopo Mbezi Beach Jijini Dar Es Salaam.

Meneja wa Kanda ya Kinondoni wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bi Zahara Kayugwa akitoa mada wakati wa semina iliyoandaliwa na Mfuko wa Penhsheni wa PPF kwaa Waajiri wa Makampuni na mashirika mbalimbali iliyofanyika katika ukumbi wa Seaescape, Mbezi Beach Jijini Dar Es Salaam leo.

Mgeni Rasmi Prof Betria Mapunda akiwa katika picha ya Pamoja na Waajiri pamoja na wafanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF leo katika Semina iliyoandaliwa na Mfuko wa Pensheni wa PPF iliyofanyika Katika Ukumbi wa Seascape Hotel Mbezi Beach Jijini Dar.
Meneja wa Kanda ya Kinondoni wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bi Zahara Kayugwa akiwaelezea waajiri waliohudhuria semina iliyoandiliwa na mfuko wa pensheni wa PPF leo jinsi kanuni mpya inavyofanya kazi kwa wanachama ili kuweza kupata mafao yao kutoka mfuko wa pensheni wa PPF.
Baadhi ya waajiri wakielekeza kuhusu jinsi ya kuweka mfumo wa PPF Taarifa katika simu zao za Smartphone leo katika semina iliyofanyika katika Ukumbi wa Seascape hotel Mbezi beach Jijini Dar Es Salaam.

Majaliwa E Mkinga, Mchambuzi na Mtengenezaji wa Mifumo ya Teknolojia ya habari na mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa PPF akielezea jinsi PPF ilivyotengeneza mfumo wa kupata taarifa za wanachama kupitia simu aina za Smartphone na kuutaja mfumo huo kuwa ni PPF TAARIFA App ambayo mteja ataweza kuiweka katika simu yake ya mkononi.

Mmoja wa waajiri akiuliza swali kwa Meneja wa Kanda ya Kinondoni wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bi Zahara Kayugwa (hayupo pichani) wakati wa semina iliyoandaliwa na mfuko wa pensheni wa PPF iliyokuwa na lengo la kuwaelimisha waajiri kuhusiana na huduma mbalimbali za PPF ikiwemo huduma mpya ya PPF Taarifa App.Picha zote Na Josephat Lukaza - Lukaza Blog

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni