.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 15 Septemba 2014

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI AZINDUA RASMI TOVUTI YA JESHI LA MAGEREZA LEO JIJINI DAR ES SALAAM


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe akiwasili Makao Makuu ya Jeshi la Magereza tayari kwa uzinduzi rasmi wa TOVUTI ya Jeshi la Magereza(wa kwanza kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja akisalimiana na Mhe. Waziri(wa pili kulia) ni Kamishna wa Huduma za Urekebishaji, Deonice Chamulesile(kushoto) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa.


Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja(aliyesimama) akitoa maelezo mafupi kabla ya uzinduzi rasmi wa TOVUTI ya Jeshi la Magereza leo Septemba 15, 2014 katika Viwanja vya Ofisi ya Makao Makuu ya Jeshi la Magereza.


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe akitoa hotuba kwenye hafla ya uzinduzi wa TOVUTI ya Jeshi la Magereza, leo Septemba 15, 2014 Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe akikata utepe kabla ya kuzindua rasmi TOVUTI ya Jeshi la Magereza inayopatikana kupitia annuani ya www.magereza.go.tz(wa pili kulia) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja.


Muonekano wa Mwanzo wa TOVUTI ya Jeshi la Magereza inayopatikana kupitia annuani ya www.magereza.go.tz (Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni