Rais Wa Zanzibar na Mwenyekiti Wa Baraza La Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiaana na Balozi Comoro Nchini Tanzania alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Comoro akiwa katika Ziara Ya Kiserikali akiwa amefuatana na Mkewe Mama Mwanamwema Shein Na Viongozi Mbali Mbali.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akipunga mikono kwa Wananchi wa Comoro akiwa na Makamo wa Kwanza wa Rais wa Comoro,Mohamed Ali Soilihi Wakati wa mapokezo alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Comoro leo akiwa katika Ziara ya Kiserikali.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na Mkewe Mama Mwanamwema Shein pamoja na Makamo wa Kwanza wa Rais wa Comoro,Mh. Mohamed Ali Soilihi wakiangalia Ngoma za Utamaduni mara walipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Comoro leo akiwa katika ziara ya Kiserikali.[Picha Na Ramadhan Othman,Ikulu Zanzibar.]
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni