Makumi ya wanawake na wasichana
kutoka katika vijiji viwili kaskazini mashariki mwa jimbo la Adamawa
nchini Nigeria wametekwa na wapiganaji wa kundi la Boko Haram.
Taarifa za utekaji huo zimetolewa na
wakazi wa vijiji hivyo ingawa hadi sasa mamlaka za serikali
hazijathibitisha.
Wakazi wa vijiji hivyo wamesema
tukio hilo limetokea siku moja tu kupita jeshi la Nigeria tangu
kutangaza kusitisha mapambano na Boko Haram, katika kujaribu kuachiwa
huru wasichana 200 iliowateka mwezi Aprili.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni