Schumacher akiwa na mkewe Corinna
Daktari wa Ufaransa aliyemtibu
bingwa wa mbio za magari za Langalanga Michael Schumacher baada ya
kupata ajali wakati akiteleza kwenye barafu, amesema anaweza akapona
ndani ya miaka mitatu.
Daktari Jean-Francois Payen, wa
hospitali ya Grenoble alimtibu Schumacher baada ya kuumia Desemba
2013, ameitembelea familia ya Schumacher katika nyumba yao iliyopo
nchini Switzerland.
Schumacher (45) anatibiwa akiwa
nyumbani baada ya kukaa miezi sita akipatiwa tiba bila ya fahamu
kufuatia ajali hiyo aliyoipata huko Meribel nchini Ufaransa.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni