.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 20 Oktoba 2014

POLISI MKOANI ARUSHA WAMUUA KWA KUMPIGA RISASI MTUHUMIWA WA MATUKIO YA ULIPUAJI MABOMU

                                                                                 IGP Ernest Mangu
Na, Mwandishi wetu

Kiongozi wa watuhumiwa urushaji mabomu nchini na umwagaji tindikali, Yahaya Hassan Omari Hela maarufu kwa jina la Yahaya Sensei (31) mkazi wa Mianzini Jijini Arusha, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo,baada ya kupigwa risasi na Polisi eneo la mguu na tako la kulia, wakati alipojaribu kuruka ndani ya gari la Polisi kwa lengo la kutoroka.

Akizungumza leo na waandishi wa habari Jijini Arusha, kamanda wa Polisi, Liberatusi Sabas, amesema polisi walimuua Oktoba 19 mwaka huu majira ya saa 5:30 Usiku huko eneo la Kisongo, Wilayani Monduli, katika barabara ya Arusha-Babati, wakati wakielekea kijijini kwake, alikozaliwa Chemchem Wilayani Kondoa, Mkoani Dodoma kwa lengo la kwenda kuonyesha bomu lililoko huko.

Amesema kuwa mtuhumiwa huyo alikuwa mwalimu wa Karate na Judo na alikuwa muasisi na kinara wa matukio ya ugaidi yaliojitokeza Jijini Arusha, Zanzibar, Mwanza na Dar es Salaam.

Sabas amesema kupatikana kwa marehemu huyo kumetokana na Intelejensia imara ya Polisi ya kisasa na ya hali ya juu na walimkamata Mkoani Morogoro Oktoba 6 mwaka huu,na kusafirishwa Oktoba 11 mwaka huu kuletwa Jijini Arusha, na alipohojiwa alikiri kuhusika na kuratibu matukio mbalimbali ya ugaidi na alikuwa kijificha kwenye nyumba tofauti na porini.

Amesema kuwa Mtuhumiwa huyo alipigwa risasi kwenye mguu wa kulia na kalio la kulia pale alipojifanya kutumia uzoefu wake wa Judo na Karate na alipokimbizwa Hospitali ya Mkoa kwa matibabu alifariki njiani na mwili wake umehifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti hospitalini hapo.

Sabas amesema baada ya kumkamata ametaja baadhi ya matukio tisa aliyoshiriki kufanya ya umwagaji tindikali kwa baadhi ya watu na urushwaji wa mabomu maeneo mbalimbali likiwemo la Mei 5 mwaka 2013 saa 10:30 maeneo ya Kanisa la Roman Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi lililopo Olasiti Jijini Arusha, ambapo aliratibu kurushwa kwa bomu na kusababisha vifo vya watu watatu na majeruhi 56.

Hata hivyo Kamanda alisema bado wataendelea kuwakamata wengine wadogo wadogo waliopo katika kikundi hicho ambao amewataja na amesema marehemu amekiri kuendesha Karate na Judo kwenye baadhi ya Misikiti Jijini Arusha, ila kwa sasa hakuna tena kazi hiyo kutokana na Polisi kusambaratisha kikosi chote.
Mwisho

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni