.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 30 Oktoba 2014

WAANDAMANAJI WACHOMA MOTO BUNGE BURKINA FASO KUPINGA RAIS KUONGEZEWA MUDA

Waandamanaji waliokerwa na mipango ya kumruhusu rais wa Burkina Faso, Blaise Compaore kuongeza muda wake wa utawala wa miaka 27, wamechoma moto bunge.

Mashuhuda wamesema katika Jiji la Ouagadougou, jengo la Jiji na Makao Makuu ya chama tawala pia nayo yamechomwa moto.

Vikosi vya ulinzi vimerusha mabomu ya machozi kutoka kwenye helkopta, wakati kundi la watu likielekea makazi ya rais.

Wabunge wamesitisha zoezi la upigaji kura ya kuridhia rais Compaore kuwania tena kiti cha urais katika uchaguzi mkuu.
                             Waandamanaji wenye hasira wakionyesha hasira zao

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni