Rubani huyo alikuwa airushe ndege hiyo kutoka uwanja wa ndege wa Newquay kuelekea London Gatwick, kabla ya wasaidizi wake kutoa taarifa polisi kuwa amelewa chakari, hali iliyowalazimu polisi kumshusha na kwenda kumfanyia kipimo cha ulevi na kumfungulia mashitaka.
Kufuatia tafrani hiyo iliyotokea jumatano, safari ya ndege hiyo ilifutwa kwa muda hali iliyosababisha abiria waliokuwa wanasafiri na ndege hiyo kuchelewa kuunganisha ndege nyingine kuendelea na safari zao.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni