.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 20 Oktoba 2014

WAZIRI WA VIWANDA JAPAN AJIUZULU KWA KUTUMIA FEDHA ZA KAMPENI KUNUNUA VIPODOZI

Waziri wa Viwanda na Biashara Yuko Obuchi amejiuzulu kufuatia madai kuwa alitumia vibaya fedha za shughuli za kisiasa, jambo ambalo limeelezwa kuwa ni pigo kwa Waziri Mkuu Shinzo Abe.

Waziri huyo Yuko Obuchi anadaiwa kutumia fedha za kundi lake la kisiasa pamoja na michango mingine katika kununua vipodozi pamoja vitu visivyohusiana na siasa.

Waziri Obuchi amewasilisha barua yake ya kujiuzulu kwa Bw. Abe katika mkutano wao uliodumu kwa dakika 30.

Wachambuzi wa mambo wanasema kujiuzulu kwa Obuchi kunadhohofisha jitihada za Bw. Abe za kuwapatia nafasi za uongozi wa juu wanawake zaidi.
 Waziri Abe ameshapoteza mawaziri wawili wanawake kati ya watano aliowateuwa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni