Bibi mwenye umri wa miaka 91
amewashangaza wafanyakazi wa chumba cha maiti Jijini Warsaw nchini
Poland baada ya kuzinduka akiwa ndani ya mfuko wa kuhifadhia maiti
saa kumi na moja kupita tangu alipotangazwa kuwa amefariki duni
nyumbani kwake.
Televisheni ya nchi hiyo imemtaja
bibi huyo kuwa ni Janina Kolkiewicz ambaye aliinuka akiwa ndani ya
mfuko wa kuhifadhia maiti katika chumba cha maiti chenye ubaridi
mashariki mwa Poland hapo jana.
Daktari Wieslawa Czyz
aliyethibitisha kifo hicho aliiambia Televisheni hiyo kuwa alikuwa na
uhakika kuwa bibi huyo alikuwa amekufa na kuongeza kuwa ameshangazwa
na kuwa haelewi kilichotokea kwani moyo wake ulisimama na alikuwa
hapumui, polisi imeanza uchunguzi wa tukio hilo.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni