Viongozi wa dunia wameanza kuwasili
nchini Australia kwa ajili ya mkutano wa G20 mwishoni mwa wiki hii
unaofanyika kwenye Mji wa Queensland huko Brisbane.
Mkutano huo wa siku mbili
unaohudhuriwa na marais wa Marekani, China, Urusi na wengineo,
utajadili katika kusaidia ukuaji.
Waziri Mkuu wa Australia, Tony
Abbott amesema viongozi hao watajadili suala la kuongeza ajira,
kubaini udanganyifu katika ulipaji kodi, na kuimarisha uchumi wa
dunia.
Hali ya mgogoro uliopo baina ya
Urusi na Ukraine pia unatarajiwa kujadiliwa, huku wanaharakani
wakitaka mabadiliko ya hali ya hewa yawe ndio agenda kuu.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni