Wanaharakati zaidi ya 200 wamefukia
vichwa vyao kwenye mchanga katika fukwe ya Bondi, kuonyeshwa kukerwa
kwao na kutochukuliwa hatua suala la mabadiliko ya Hali ya Hewa.
Wanaharakati hao wamefanya hatua
hiyo wakati viongozi wa dunia wakiwasili Australia katika mkutano wa
G20 utakaofanyika wikiendi hii huko Brisbane.
Waziri Mkuu wa Australia Tony Abbot
amekosolewa kwa kutohusisha suala la mabadiliko ya Hali ya Hewa
katika agenda ya mkutano huo.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni