Mshambuliaji mahiri wa Arsenal, Alexi's Sanchez akiifungia timu yake bao la pili.
Wakicheza nyumbani katika uwanja wao wa Emirates, washika bunduki wa London, Arsenal usiku wa kuamkia leo wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Borussia Dortmund toka Ujerumani katika mchezo wa ligi ya mabingwa Ulaya.
Katika mchezo huo, Arsenal walijipatia bao la kwanza kupitia kwa mshambuliaji wake Yaya Sanogo katika dakika ya pili ya mchezo, bao ambalo lilidumu hadi kipindi cha kwanza kinamalizika.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na Arsenal kujipatia bao la pili kupitia kwa Alexi's Sanchez katika dakika dakika ya 57 na kuamsha furaha kwa mashabiki wa Arsenal ambao walikuwa wakiishangilia timu yao mwanzo mwisho.
Sanogo akiifungia timu yake bao la kwanza katika dakika ya 2 ya mchezo huo dhidi ya Borussia Dortmund usiku wa kuamkia leo.
Matokeo mengine ya michezo ya ligi ya mabingwa Ulaya iliyochezwa usiku wa kuamkia leo ni kama ifuatavyo:-
Atletico Madrid 4 vs 0 Olympiakos
Malmo FF 0 vs 2 Juventus
Ludo 2 vs 2 Liverpool
Zenit 1 vs 0 Benfica
Bayer 04 Leverkusen 0 vs 1 Monaco
Anderlecht 2 vs 0 Galatasaray
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni